- Back to Home »
- BBC »
- Kuhusu mama aliyemtelekeza mtoto wake ndani ya karatasi.
Shirika la habari la BBC limeripoti kuwa, Mwanamke mmoja
aliyemtelekeza mwanawe ndani ya karatasi ya plastiki katika bustani moja
nchini Uingereza amenusurika na adhabu ya kifungo jela.
Mtoto huyo mchanga aliyekuwa wa siku moja tu, alikutwa na mtu aliyekuwa anamtembeza Mbwa wake katika bustani hilo.
Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 27, alihukumiwa kifungo cha nje
cha miezi sita na kuwekwa chini ya ulinzi wa maafisa wa kijamii kwa
miaka miwili.
Hata hivyo alikiri kumtelekeza mtoto wake kwa makusudi na kusema kuwa
aliathirika kimawazo baada ya kujifungua mtoto huyo mwezi Mei.
Polisi walisema kuwa mtoto huyo alinusurika kifo kwa dakika
thelathini tangu kutelekezwa kwani alipatikana haraka sana na kwamba
mwili wake tayari ulikuwa umeanza kuwa baridi.
Mtoto huyo alipatikana mwaka jana akiwa amefungwa ndani ya taulo na kuwekwa ndani ya karatasi ya Plastiki katika bustani hilo.
Mama huyo aliambia mahakama kuwa alifanya kitendo chake katika hali ya kutojielewa.
Pia alifahamisha mahakama kuwa alijifungulia mtoto wake katika sakafu
ya bafu nyumbani kwa mamake hali ambayo ilimuathiri kimawazo.
Alificha ujauzito wake kutoka kwa familia yake na pia hakuwahusisha
madaktari kwa sababu alihofia kuwa hangeweza kustahamili ujauzito wake.