- Back to Home »
- CHEKA NA MKWELE »
- {Vichekesho} Juma kavamia sherehe ya harusi ya wanyakyusa
Posted by : MKWERE ORIGINAL
Alhamisi, 8 Agosti 2013
Jamaa mmoja aitwaye JUMA alivamia sherehe ya harusi ya wanyakyusa na kujifanya mwanafamilia wa bwana harusi. Wakati wa utambulisho wa ndugu wa bwana harusi wakaanza kusimama mmoja mmoja na kutaja jina lake....
Wa kwanza akasema: Naitwa MwakalebelaWa pili akasema: Naitwa Mwakipesile
Wa tatu akasema: Naitwa Mwakasungura
Wa nne akasema: Naitwa Mwasomola
Wa tano akasema: Naitwa Mwakatundu
Ilipofikia zamu ya Juma akafikiriaaa kisha akadhani kuwa kila jina katika kabila lile ni lazima uanze na “MWA”, basi akainuka kwa makonfidensi na kupaza sauti “naitwa MWAJUMA“