- Back to Home »
- CHEKA NA MKWERE »
- TAMKO LA RASMI KUHUSU URAIA PACHA KUTOKA KWA WATANZANIA WAISHIO WASHINGTON DC
Posted by : ujugu
Jumamosi, 12 Aprili 2014
Tunapenda Kutoa Tamko Rasmi kwa Bunge la Katiba na Serikali kutoa haki
ya Uraia kwa Watanzania Wote popote walipo Duniani. Uraia Wa Mtanzania
aliezaliwa Tanzania na Kizazi chake usijali hali na mahala alipo
Mtanzania Huyo.
Kutokubaguliwa kwetu kwenye swala hili la Haki ya Kuzaliwa na Kuruhusiwa
kwa Uraia Pacha kwa Waliozaliwa Tanzania na Vizazi vyao ni muhimu
katika kuimarisha nchi, kutoa haki kwa Watanzania wote waliozaliwa
Tanzania pamoja na vizazi vyao. Haki ya kuzaliwa kwa watanzania wote
kutaimarisha Zaidi mahusiano kati ya watanzania tulio nje na serikali
yetu tukufu.
Watanzania Hapa Washington, DC na tulio nje tumekuwa mbele kuitangaza
nchi yetu, kuiwakilisha nchi yetu na kuibeba Bendera ya Tanzania huku
nje . Watanzania tumekuwa tukishirikiana na Viongozi wa nchi yetu
wanapokuja huku nje kwenye mambo mbalimbali ya kimaendeleo, kijamii na
kielimu ili kuhakikisha nchi yetu inasonga mbele.
Watoto wetu waliozaliwa huku nje wamekuwa wakiimba nyimbo ya Taifa la
Tanzania wanapokuja viongozi mbali mbali huku na kwenye shughuli mbali
mbali za kitaifa na kimataifa ambazo huwa tunaiwakilisha nchi yetu huku
ugenini.
Watanzania wenye uraia wa Tanzania na Wale waliochukua Urai wa Hapa ,
pamoja na watoto wao waliozaliwa hapa ambao ni Wamarekani kwa kuzaliwa
tunajisikia na tunaipenda Tanzania kama wenzetu walioko Marangu au
Kimanzichana. Tofauti iliyopo ni kwamba sisi tuko huku na wenzetu wako
Biharamulo. Watoto wetu wamezaliwa hapa na Binamu zao wamezaliwa
Chalinze. Sisi sote na watoto wetu ni watanzania na tunataka
tutambulike na kuwa na haki sawa.
Watanzania wa Washington DC, tumekuwa tukishirikiana kwa hali na mali na
Ubalozi wa Hapa kuitanganza nchi yetu na kuitetea na kuiletea sifa
nzuri Tanzania. Hivi Sasa Ubalozi wetu hapa Unaandaa sherehe za Miaka 50
ya Muungano na Ni sisi Watanzania wa Ughaibuni tutashiriki kwa Moyo
Mmoja na nguvu zote kuipeperusha bendera ya Tanzania kwa niaba ya nchi
nzima. Watato wetu wataonyesha utamu wa nyimbo ya Taifa la Tanzania.
Viongozi wa Taifa watazungumza na watanzania wa hapa na kujadili
maendelea na muelekeo wanchi. Sisi Ni Watanzania.
Tanzania Itajengwa Na Watanzania. Sisi Na Vizazi Vyetu Huku Ughaibuni ni Watanzania.
Iddi Sandaly,
Rais Wa Jumuiya Ya Watanzania ,
Washington DC, Maryland na Virginia.